MITANDAO HII ITUMIKE IPASAVYO

MITANDAO HII ITUMIKE IPASAVYO

Hivi ni mara ngapi umewahi kuandika barua pepe kwenda kwenye anuani ya taasisi Fulani ya elimu ukakuta kumbe haifanyi kazi haswa hizi za mawasiliano kwa wote kama info@maishabora.ac.tz sio vyuo tu hata taasisi na mashirika ya umma kote huko kumekuwa na matatizo sawa .

Au hata ni mara ngapi kuona mawasiliano ya kiofisi ambayo inayo anuani zake pepe zikitumia anuani zingine za kusajili bila kupitia anuani za tovuti zao ? pamoja na kupiga kelele kwa kipindi kirefu sana inaonyesha watu hawasikii na hawataki hata kubadilika kwenda na wakati.

Kwa kipindi kirefu kidogo nimekuwa mmoja wa wale watu wanaoshangaa kwanini vyuo vikuu nchini havina au havijaanzisha huduma za mawasiliano kwa njia ya mtandao kwenye tovuti zao zinazohusu miradi Fulani au vikundi Fulani vya wanafunzi ?

Kwa mfano chuo kikuu cha maisha bora wiki hii darasa jipya limeanza na walimu wa darasa hilo wameamua kufungua group kwenye google ambapo wameweka anuani pepe za wanafunzi wao kwa ajili ya kuwasiliana nao na kubadilishana vitu mbalimbali vinavyohusu masomo yao .

Nimeamua kwenda kwenye mtandao wa maisha bora nimeshangaa kwa mfano wanafunzi wa chuo hicho hawana maelezo ya kutosha hata kuhusu group yao hiyo mbali na kujulishwa kwamba ile ni mali ya yahoo chochote kinachobadilishwa mule ni mali ya yahoo , hata chuo chenyewe hakina sera za mawasiliano kwa njia ya mtandao na hata maelezo mengine ya jinsi wanafunzi wanavyowasiliana wenyewe hata walimu kwa walimu wenyewe .

Mfano wa chuo cha maisha bora ni mfano halisi wa vyuo vingine na taasisi za elimu , mashirika ya ummah na yale yote yanayofanya kazi kwa maslahi ya nchi wote wameamua kwa makusudi kabisa kujiingza kwenye kundi hili kufungua groups kwenye yahoo au google kwa ajili ya mipasho yao ya kikazi hata kama sio public lakini ni vitu ambavyo mtu anaweza kutafuta kutumia search engine mbalimbali na kuweza kujua kinachojadiliwa ndani .

Na pia wengi wanasajili bila kupitia kwa makini maelezo kuhusu matumizi ya mitandao hiyo kama inaendana na maslahi yao kwa namna Fulani au la , hili ni suala la kuangalia kwa karibu zaidi , tujenge utamaduni wa kuwa na vyetu wenyewe .

Kuna hitajika jitihada za dhati kabisa kwa wadau popote walipo wahakikishe kwamba wanaandaa sera za mawasiliano kwenye vitengo vyao vya kazi vinavyohusu ICT ndani yake kuwe na mkataba ambapo kila mfanyakazi anayekabidhiwa kifaa hicho anaweza kuweka sahihi yake na kukubaliana na matakwa ya shirika , chuo au taasisi yake .

Vyuo hivi , mashirika na taasisi zianzishe vikundi hivi kupitia wavuti zao wenyewe hii ni kwa maslahi yao na nchi kwa ujumla , makosa ambayo yamefanyika huko nyuma kuacha mambo haya yasirudiwe tena huu ni mwaka mpya tunaingia kwenye ushindani wa kila aina kwahiyo ni vizuri basi taasisi , vyuo na taasisi zijue wajibu wao katika ushindani hii .

Nawatakia mafanikio tele katika kuanzisha sera za mawasiliano kwenye taasisi , mashirika na sehemu zingine za kazi pamoja tunaweza kwanini wao waweze sisi tushindwe .

Haturudi Nyuma


Yona Fares Maro
I.T. Specialist and Digital Security Consultant

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *